Baada ya shiloleh, Ndoa ya stamina yanukia.

Msanii wa bongo fleva Stamina,ameamua kuuvua ukapela na kuamua kujiunga katika kundi la kuanzisha familia, msanii huyo jana aliamua kuchukua hatua hiyo na kumvalisha pete ya uchumba mwanamke aliyekuwa nae katika mahusiano kwa muda mrefu sasa.

download latest music    

Stamina katika tukio la kumvisha pete mkewe mtarajiwa.

Inakuwa ni jambo la kheri kwa wasanii wa bongo kuamua kujiingiza katika maswala ya familia ukizingatia wao ni vioo vya jamii lakini pia umri pia unakwenda hivyo ni lazima kujikita huko pia.

kwa kipindi hiki cha mwisho wa mwaka imekuwa ni kama muda muafaka kwa wasanii na watu watasnia ya sanaa bongo maana kumekuwa na mfululizo wa matukio ya ndoa na kuvishana pete kwa wasanii wengi wakiamua kuacha ukapela na kuanzisha familia.

Mwaka huu umekuwa wenye kheri baadaya wasanii kadhaa kufunga ndoa ikiwepo Masanja Mkandamizaji, Joti,RomMy johnson,shiloleh na wengine kibao.

Stamina anaetamba na kibao cha Kiba100 alichoimba na msanii mwenzie Roma ambao wanaunda kundi la Rostam amemvisha pete ya uchumba mpenzi wake hivyo tutarajie ndoa yao hivi karibuni.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.