Baadhi Wamshambulia Joyce , ni Baada ya Kujitokeza Kwa Waliotelekezwa.

Baadhi ya watu wamejikuta wakimtolea povu mwanamama ambae alianza kama utani katika tasnia ya filamu kwa kuwainua wasanii na mpaka kuja kuwa na kipindi chake ambacho kilikuwa kikiwatetea wanawake kilichojulikana kama wanawake live.

Siku ya jana wanawake wengi walijitokeza katika ofisi za Mh mkuu wa mkoa baada ya mkuu wa mkoa kujitolea kuwasaidia wanawake wote walio na shida ya kutelekezwa na wanaume wa kwa kuwazalisha na kushindwa kulea watoto.

download latest music    

Kuna picha zilisambaa sana baaada ya mwana dada Joyce Kiria kujitokeza katika umati huo wa wanawake akiwa ni mmoja wa waliokwenda kwa ajili ya kutaka msaada.

Hata hivyo bado hakuna haja ya watu kubaki mdomo wazi kumuona Joyce Kiria katika eneo hilo kwa sababu kipindi cha nyumba joyce alishawahi kuweka wazi maisha yake ya ndoa na kusema kuwa ameshindwa kukaa kwenye ndoa hivyo ameamua kuachana na mwanaume wake. inawezekana pia uwepo wake ni kwa ajili ya kutaka msaada lakini pia inawezekana yuko pale lwa sababu yeye pia ni mwanaharakati wa akina mama hivyo bado anamchnago mkubwa katika jamii.

Baadhi ya mashabiki wamemtukana sana na hata kumshambuia katika mitandao ya kijamii kuhusu kuwepo kwake pale, lakini akiwa kama mmoja wa wanawake jasiri Joyce siku zote amekuwa akisema haogopi kuonekana kituko mbele za watu kwa yale anayoyafanya ilimradi yanampa nguvu na kumuinua.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.