Baba Diamond Kafunguka Ishu Ya Mama Diamond Kuolewa “Msiniingilie na Mama Diamond”

Baba mzazi wa Msanii Diamond Platnumz, Mzee Abdul Juma amefunguka kuhusiana na suala linalo kiki mjini kwa hivi sasa suala la Mama mzazi wa Diamond Bi. Sandrah kuolewa na kiben-10 anayejulikana kama Shamte.

Baba Diamond na Mama Diamond inasemekana kuwa waliachana miaka mingi iliyopita baada ya kumuacha na kumtelekeza na mtoto mdogo lakini kutokana na maelezo yake inaelekea hata kama baba Diamond hana uhusiano mzuri na mwanaye Diamond lakini anaelewana na mzazi mwenziye Bi Sandra.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyoyafanya na Millard Ayo Mzee Abdul alionyesha kukasirishwa na maswali aliokuwa anaulizwa kuhusu ndoa iliyofungwa kati ya Bi. Sandrah na Shamte:

Kwanza naomba niseme kuwa sijapenda na wala sipendi kuulizwa maswali hayo yanayo muhusu Mama Nasibu kwani mimi ninavyoona kuwa yule ni mama na mwanamke mwenye nguvu zake na uwezo wake na mwenyezi Mungu kampa pumzi kaamua na kajisikia mwenyewe kuwa anahitaji mume na ana uwezo wa kumudu kuwa na mume mimi naona hakuna matatizo yoyote ila naomba niseme na niwaambie watu wote kuwa wasipende sana kuniingilia maswala yangu na mimi na Mama Nasibu mimi naona kama wana maswali wanataka kumuuliza basi wamfuate tu wenyewe wakamuulize na kama wana maswali kwa Nasibu wawafuate wenewe wawaulize kuliko kunifuata mimi kuniuliza mambo yao wanayofanya mimi sijui”.

Baba Diamond amesisistiza kuwa yeye na Mama Diamond wanaelewana kama wazazi tu ila kwa sasa wamebaki kama dada na kaka tu ambao wanasaidiana kifikra na kimawazo na pia kimaisha lakini wanaelewana vizuri.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.