Baba Dimpoz Aibuka na Kumchagulia Mwanaye Mke Wa Kuoa

Baba wa Msanii wa Bongo fleva Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz, Faraji Nyembo ‘Baba Dimpoz’ ameibuka na kumchagulia mwanaye mke wa kuoa kuangalia sifa na tabia.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Baba Dimpoz alisema vijana wengi siku hizi wamekuwa wakiwachagua wanawake wa kuoa kwa kuangalia maumbile ya nje, jambo ambalo siyo sawa kwani watajikuta wanajuta baadaye wakishaingia kwenye ndoa.

download latest music    

Lakini pia aliendelea kusema kwa upande wa mwanaye Dimpoz anamshauri akifikia muda wa kuoa aangalie mwanamke mwenye hofu ya Mungu, yaani mcha Mungu, mwenye akili ya maisha, busara na familia anayotokea na asiangalie shepu na sura kwani atakuja kujilaumu baadaye.

Unajua Dimpoz kwa mama yake yuko peke yake na mama yake alishafariki dunia hivyo anatakiwa akitaka kuoa amtafute mwanamke mwenye hofu ya Mungu ambaye atakuwa faraja kwake, atakuwa mke bora pia kwa upande mwingine awe kama mama kwake na asiangalie shepu, sura au ustaa.

Tatizo la vijana wa siku hizi wanapenda sana kuangalia sura na shepu hata wakishauriwa vipi wanaona ni ujinga, lakini cha muhimu wanachotakiwa kuangalia wanapochagua wake waangalie wacha Mungu na wenye tabia njema”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.