Baba Lulu: Sipokei Posa Ya Mtu Kwaajili Ya Binti Yangu

Baba mzazi wa muigizaji wa bongo movie Elizabeth Michael ‘Lulu’, anayejulikana kama Mzee Michael Kimemeta amefunguka kuwa hataki posa kutoka kwa mwanaume yoyote.

Lulu ambaye kwa hivi sasa yupo kwenye kipindi kigumu kutokana na kesi ya kumuua bila kukusudia aliyekuwa mpenzi wake marehemu Steven Kanumba, lakini moja kati ya watu ambao wameonekana karibu kabisa na Lulu ni baba yake. Ambapo ni juzi tu Lulu alipokuwa anakimbizwa na waandishi wa habari Baba Lulu alichukua nafasi ya ubodigadi kumlinda binti yake.

download latest music    

Katika mahojiano aliyoyafanya na kituo cha televisheni cha East Africa, Baba Lulu alifunguka yafuatayo kuhusu posa ya binti yake:

Unajua suala la ndoa ni la watu wawili yule anayeoa na yule anayeolewa, mwanaume yoyote atakayemleta Lulu sisi tutampa baraka zetu, suala la poss halipo kabisa kwenye msamiati wangu! Siuzi mtoto wangu wala sitaki posa yoyote posa yangu ni amani ndani ya nyumba yao, ndio posa watakayonipa”.

Baba Lulu alipoulizwa kama anajua uwepo wa mkwe wake anayeitwa Majjizo alisema hamfahamu kwani hajatambulishwa na binti yake lakini pia aliwasihi wananchi wasimuhukumu Lulu bure bali wasubirie sheria ichukue mkondo wake kwani mahakama ndio itakayoamua Kama Lulu ni Ana hatia ama hana hivyo amewasihi watu wasubiri hukumu ya mahakama itakayotolewa hivi karibuni ambayo itaamua hukumu ya Lulu.

 

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.