Baba Mzazi Wa Ommy Dimpoz Amtaka Mwanaye Asimzike Akifa

Baba mzazi wa Mwanamuziki wa Bongo fleva Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ anayejulikana kama Mzee Faraji Nyembo ametoa dukuduku lake la moyoni na kusema hata akifa leo mwanaye huyo asimzike.

Kwa taarifa iliyotolewa na gazeti la Risasi Mchanganyiko zimedai kuwa mzee huyo alifikia hatua ya kuongea maneno huku akidai kuwa mwanaye huyo hajawahi kumjali kwa lolote kabla na hata baada ya kuwa staa.

download latest music    

Ommy Dimpoz ni moja kati ya wasanii wa Bongo wanaojulikana kwa kula bata refu ndani na nje ya nchi ni wiki iliyopita tu Ommy alikuwa anarusha picha mtandaoni akiwa nchini Uingereza huku akihudhuria mechi ya Man United Vs Tottenham iliyofanyika katika uwanja wa Wembley stadium.

 

Kwa taarifa iliyotolewa na gazeti hilo imedai kuwa Baba mzazi wa Ommy Dimpoz anaishi mkoani Tabora katika lindi la umaskini huku maisha yake yakitegemea kuendesha bajaji:

Hivi mna habari kuwa baba mzazi wa Ommy Dimpoz ana maisha magumu sana huku Tabora? Kwa taarifa yenu huyu mzee anaishi kwa kubangaiza Kwenye bajaji tofauti kabisa na jina alilonalo mwanaye ambaye ana uwezo kabisa wa kumsaidia baba yake akaishi maisha mazuri”.

Baba mzazi wa Ommy Dimpoz akipata mihogo kwa Mama ntilie

Baada ya taarifa hizo gazeti hilo lilifanya jitihada za kumsaka Baba Ommy na kuongea naye ambaye alifunguka mazito juu ya mtoto wake huyo;

Hakuna kitu kikubwa duniani kama kuletwa duniani…Hayo mengine ya kuwa alilelewa na upande tu wa mama ni madogo tu hivyo sina kosa kwa sababu nilishamleta duniani na ninamshukuru Mungu kwa kunipa nguvu ya kufanya kazi kwani nina bajaji niliyonunua mwenyewe nina miaka 64 lakini bado napambana”.

Lakini pia Baba Ommy aliendelea kufunguka na  kusema:

Kwa mfano nikifa leo ni bora huyu Ommy asinizike au kuja Tabora maana kwanza watu watampiga na kwanza atasema ni nani wake amefariki maana  hivi niko hai hana ushirikiano”.

Baada ya maongezi hayo gazeti hilo lilimtafuta Ommy kwa njia ya simu ambapo simu iliita bila ya kupokelewa na alipotumiwa ujumbe mfupi kwa njia ya WhatsApp alijibu “Nipo Hospitalini”.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.