Babu Tale akerwa kwasababu mke wake ashindwa kupata ajira

Meneja wa Diamond- Babu Tale amekerwa na hali ya maisha Tanzania – ukosefu wa ajira ndo chanzo cha Babu Tale kuikemea serikali.

Babu Tale amesema kuwa amejaribu kutumia kila mbinu kumtafutia mkewe ajira lakini mbaka sasa hajafanikiwa licha ya kuwa na shahada.

download latest music    

Meneja huyo alisema kuwa shahada aliyopata mkewe imesalia kabatini nyumbani kwani ameshindwa kupata ajira kabisa.

“Msomi wangu bado yupo nyumbani na degree yake ipo kabatini nakumbuka nilisema ajira kamlete ila kwake imekua ngumu pamoja na connection zote nilizo nazo bado mtiani na hivi serikali imetangaza juu ya miaka 30 ajira hakuna pesa yangu imeenda bure IFM ?????” Babu Tale aliandika kwa Instagram.

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere