Babu Tale- Sijaenda South Africa Kurudisha Penzi la Diamond na Zari

Meneja wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz, Babu Tale amefunguka na kudai hakuenda nchini South Africa Kurudisha Penzi la Diamond na Zari.

Wikiendi iliyopita habari ya mjini ilikuwa Zari na Diamond baada ya video ya wimbo wa iyena kutoka ukiwaonyesha wawili wakifunga ndoa mwaka jana wakati bado wapenzi.

download latest music    

Babu Tale alitengeneza headlines baada ya kutangaza anaenda nchini South Africa kwa ajili ya kwenda Kurudisha Penzi la Diamond na Zari baada ya kutengana kwa zaidi ya Miezi minne sasa.

Lakini baada ya kufika nchini humo ambako ndipo Zari anaishi na watoto wake Babu Tale ameweka wazi kuwa hajaenda Kurudisha Penzi lao bali ameenda kuwapatanisha wawili hao ili waweze kulea watoto wao.

Kwenye mahojiano na Wasafi Tv, Babu Tale amesema ameona ni vyema wawili hao wakaelewana kwa manufaa ya watoto wao:

Kilichonileta  huku ni kuwasuluhisha matatizo yao wayaweke pembeni ili waweze kulea watoto wao, of course nimeongea sana na Zari nikamwambia kama mnataka kurudiana kimapenzi it’s up to you lakini mimi ningependa kuona wewe na Diamond mnapatana ili  watoto waweze kuwa karibu na nyinyi na ikitokea tupo South Africa ni rahisi kupita kusalimia watoto na kama watoto wamemiss Baba unampigia simu”.

Diamond na Zari wamekuwa na uadui fulani tangu wawili hao walipoachana Miezi michache iliyopita ambapo Zari alimtuhumu Diamond kwa kutowaona watoto wake kwa miezi mitano kutokana na wao kukosa maelewano.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.