“Bado Nampenda Nini, Akitaka Kurudi Niko Tayari”- Nay wa Mitego

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nay wa Mitego amefunguka na kuweka wazi kuwa bado anampenda sana aliyekuwa mpenzi wake na msanii mwenzake Nini.

Wiki chache zilizopita Nini aliweka wazi kuwa Mahusiano Yake na Nay wa Mitego yamefika mwisho na alidai ameamua kumuacha rapa huyo kwa madai amekuwa na michepuko mingi.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Bongo 5, Nay amefunguka na kudai bado anampenda sana Nini na kama atakuwa tayari kuwa naye Tena basi yeye Yupo Tayari.

Nay wa Mitego amekiri kuwa ni kweli alifanya makosa ambapo alikuwa ana michepuko kadhaa na Nini alipogundua alimpiga kibuti na hata alipomuomba msamaha hakutaka kumsamehe.

Nay amesisitiza kuwa bado anampenda sana Nini na kama atakuwa tayari kumsamehe hata leo hii basi Yupo Tayari kuwa naye Tena.

Nay amekiri kuwa ingawa yeye na Nini walikataa kuwa hawakuwa Kwenye Mahusiano kwa muda mrefu lakini walikuwa pamoja kwa miaka zaidi ya miwili na hata kudai walianza Mahusiano kabla hata hajajua kuwa Nini anaimba.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.