Bahati Kutoka Kenya Bado Yupo Na Lulu Kichwani Kwake

Mwanamuziki wa nyimbo za injili kutoka Kenya Bahati amekiri Elizabeth Michael maarufu kama Lulu bado anamchanganya kichwani baada ya kuharibu makubaliano yao siku za nyuma.

Bahati alishawahi kufunguka na kusema mwaka 2016 alitoka nchini Kenya mpaka Tanzania kwa ajili ya kumtaka Lulu awe Video vixen Kwenye wimbo wake unaoitwa Maria lakini alipofika hotelini ambapo walipanga kukutana kwa ajili ya kikao Lulu hakufika

download latest music    

Bahati alidai baada ya Lulu kumgeuka na kukataa kutokea mwishoni kabisa hivyo ikabidi amuweke Jokate kwenye video ya wimbo huo ingawa chaguo lake lilikuwa Lulu.

Safari hii  Bahati amerudi tena Tanzania kwa ajili ya kufanya kazi na msanii wa WCB, Mbosso, hata hivyo bado anakumbuka alichofanyiwa na Lulu.

Ilikuwa meeting ya video vixen, kama alinifanyia hivyo je anayempenda inakuwaje?, na mimi nilikuwa nimeweka shilingi kidogo, naongea kwa uchungu”.

Siku za nyuma msanii huyo alishawahi kukiri kuwa anampenda Lulu na kama angepata bahati ya kuwa naye basi bila Shaka angejiona mwenye bahati.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.