BarakaAomba Kisiwa cha Mbudya Kifungwe
Mwanamuziki Baraka The Prince amefunguka na kuishauri serikali kuwa kwa muda ambao yameshatokea matatizo mengi katika kisiwa cha Mbudya abasi ni bora kisiwa icho kingefungwa kwa muda mpaka pale kutakapo boreshwa na kuwekwa kwa huduma za msingi katika kisiwa icho.
Baraka anasema kuwa kisiwa icho kimekuwa kikiingiza pesa kwa sababu ya watu wengi wanaoenda huko hivyo uweoz wa kuweka maboresho unawezekana na kama haiwezekani basi ni bora kukifungwa kwanza.
Kisiwa hicho kimekuwa hatarishi kwa maisha ya binadamu na hata kupoteza maisha ya watu weng sana kutokana na mazingira yake kuwa hatarishi, hata hivyo wasaii wanazidi kuguswa na swala hilo kutokana na kuwa wamkuwa wakienda na kuona matukio ya vifo vya watu mara nyingi na hata hivi karibuni kupoteza producer Pancho Latino.
Malalamiko hayo yamekuwa yakitolewa na watu tofauti tofauti na sasa ni jukumu la serikali na uongzo wa kisiwa icho kurekebisha baadhi ya vitu vya muhimu ili kuokoa maisha ya watu.