Barakah The Prince alaumu siasa kwa kusababisha wimbo wake kutofanya vizuri

Barakah The Prince anadai kuwa siasa Tanzania ni moja ya vitu ambavyo vinasababisha nyimbo za wasanii kutofanya vizuri.

Muimbaji huyo amekiri kuwa wimbo wake mpya ‘Acha Niende’ aliyowachia miezi mitatu iliyopita uliathirika na kipindi cha mpito ambao umebadilisha hali ya muziki nchini.

download latest music    

Akiongea katika kipindi cha Enewz cha EATV, Barakah The Prince alisema kuwa ‘Acha Niende’ haukufika malengo ambayo alijiwekea wakati alitoa wimbo huo.

“Hali ni ngumu kweli kwa wasanii, nyimbo nyingi ambazo zimetoka hivi karibuni zimeshindwa kufanya vizuri kusema kweli hata wimbo wangu haujafikia kwenye malengo ambayo nilijiwekea wakati natoa au hata nikilinganisha na nyimbo zangu zilizopita,” Barakah The Prince alisema.

https://www.youtube.com/watch?v=IKjVsyA77II

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere