Barakah The Prince amsifu sana Diamond kuliko Ali Kiba akilinganisha mchango wao kwa muziki

Barakah The Prince anatambua kuwa Diamond and Ali Kiba ndo ndume katika ulingo wa muziki Tanzania. Lakini mwimbaji huyo amekiri kuwa Chibu Dangote ndo ndume kamili.

Barakah aliwataja wasanii watatu ambao wako na mchango mkubwa kwenye muziki; Diamond, Ali Kiba na Ommy Dimpoz.

download latest music    

Akiongea na Bongo 5, Barakah alimsifu sana Diamond ambaye alisema ameweka mfano mzuri wa kuigwa na wasanii wote nchini.

“Kwa mfano Bongo kwa mtu kama Ommy Dimpoz, Ommy ni package kabisa ya staa, Diamond ni package na Alikiba ni package iliyokabilika ambayo unaona kabisa huyu ni staa kakamilika. Kwa hiyo kwenye muonekano pia hususan mavazi na mwili lazima mtu uwe makini sana. Diamond ni miongoni mwa mtu ambaye anaowasanua sana watu kwenye vitu, nani alitegemea kama Diamond anaweza kuja na Chibu perfume? Hakuna mtu aliyetegemea, lakini jamaa kaka kafikiria watu wanapenda sana kunukia.

Baraka The Prince

“Nampongeza sana Diamond, ni mtu ambaye anatumia nafasi yake aliyopo sasa hivi vizuri. Kwa hiyo sitaki kusema kuwa watu wengi wanafanya kwa kuwa yeye kafanya, no lakini uyeye anaweza akawa anawapa watu mioyo ya kuthubutu. Unajua mtu mpaka kurizki na kuweka hela yake nyingi kwenye brand ya nguo au nini, ujue hapo umerizki na biashara ina mambo mawili, kuna kunyanyuka na kuna kuanguka.

“Mtu mpaka uweze kurizki lazima uone mfano kwa mtu, huwezi kurizki tu, kwa hiyo yeye ni miongoni mwa watu wanaowapa watu moyo na kuona kumbe kitu hiki unaweza kukifanya na kitu hiki na kikawezekana na tukabiga mitonyo na maisha yetu yakawa mazuri,” Barakah alisema.

 

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere