Barakah The Prince: Mimi Sio Mkorofi Nachukiwa Kwasababu ni Msemakweli

Mwanamuziki wa Bongo fleva, Barakah The Prince anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘sometimes’ amefunguka na kudai kuwa yeye sio mkorofi kama wasanii wenzake wengi wanavyodai bali ni msema kweli.

Barakah amekuwa akishika vichwa vya habari wiki chache zilizopita baada ya kurushiwa tuhuma mbali mbali na wasanii wenzake na mashabiki zake ambao wamekuwa wakimkosoa mara ya mara.

download latest music    

Barakah amesisitiza kuwa hajawahi kugombana na msanii yoyote ila kusema kwa ukweli ndio kunafanya watu kumchukulia kama mkorofi.

Kwenye mahojiano aliyofanya na kipindi cha XXL cha Clouds Fm, Barakah amefungukia suala hili:

Sijawahi kumtukana au kugombana na msanii but ule ukweli wangu labda unamwambia mtu, unajua watu wengi hawapendi kuambiwa ukweli anaweza akakuboa ukamwambia ukweli akakuchukulia tofauti kwa hiyo nadhani sana hiyo ndio ilikuwa inachangia, unajua wakati huu nimejitahidi ndio maana hata nimekaa kimya kwa muda mrefu sana , nimejaribu kukaa chini na watu wengi na kuzungumza nao na wamenipa canceling wakiwemo watu wakubwa kwenye entertainment”.

Mapema wiki hii Barakah aliingia kwenye bifu na mwanamuziki mwenzie Shilole kwa kile Shilole alichodai kuwa Barakah nimjeuri na mgombanisho lakini pia Barakah amegombana na uongozi mzima wa label yake ya zamani na Mc cater.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.