Barakah the Prince: Sijasimamiwa na Ali Kiba

Barakah the Prince ni miongoni wa wasanii wachache kutoka Tanzania ambao wako chini ya usimamizi wa kampuni ya RockStar4000.

Hivi juzi Ali Kiba aliteuliwa kuwa mkurugenzi katika kampuni hio ya RockStar4000.Hata hivyo Barakah amedhibitisha kuwa yeye hasimamiwi na Ali Kiba.

download latest music    

Akiongea na kipindi cha 5 Selekt ya EATV, Baraka The Prince alitoa ufafanuzi kuwa yeye ni msanii anayesimamiwa kazi zake na kampuni ya RockStar4000 na si kusimamiwa na Ali Kiba.

“Mimi sitaki sana kuzungumzia sana juu ya Alikiba kuwa Director wa RockStar4000 kwani kipindi ambacho yeye anaingia mikataba mimi nilikuwa Nairobi na wao walikuwa Afrika Kusini na sijapata nafasi kusikia chochote hivyo kwa sasa bado sijui vizuri hilo jambo, siwezi kulizungumzia japo nafahamu maana naweza kuzungumzia nikazungumza nikasema jambo lisilo la kweli. Ila nimefurahi sababu Alikiba ni kaka yangu na naishi naye vizuri na najua kuwa kazi itakwenda vizuri. Mimi ni msanii wa RockStar4000 na si msanii wa Alikiba hilo watu naomba waelewe,” alisema Barakah The Prince.

 

About this writer:

Martin Oduor

Ultimate keyboard ninja dedicated to bringing you the juiciest stories on blogosphere