Barnaba Agoma Kumhusisha Mama Steve na Nyimbo Zake za Mapenzi.
Mwanamuziki mwenye kipaji cha kuimba nyimbo za mapenzi na za kulalamika Barnaba Classic amefunguka na kusema kuwa watu wamekuwa wakihusisha sana nyimbo zake na maumivu aliyowahi kuyapata ya kuachana na mwanamke aliyemzalia mtoto, mama steve kitu ambacho kwake sio cha kweli.
Barnaba ambae kwa sasa ametoa wimbo wa tuachane mdogo mdogo, anasema kuwa kuimba nyimbo za mapenzi ni kipaji chake kila siku wala haihusiani na kitu chochote cha kuumizwa na mamsteve hivyo watu wasiwe wanahusisha muziki na kitu icho.
Tangu barnaba ameachana na mama wa mtoto wake, barnaba ameshaimba baadhi ya nyimbo zenye kuonyesha kulalamika kuumizwa na mapenzi kitu kinachowafanya mashabiki kuisi kuwa labda bado anakumbuka mapenzi ya mwanamke huyo.
siwezi kuzungumzia mzazi mwenzangu ulshawahi kuona wapi mtu anamzungumzia mtu mmoja kla siku,mimi ninawaimbia watanzania.Watu walishanza kumjua barnaba kabla ya kuingia katika mahusiano, sijaanza kuimba mapenzi leo, nafanya kazi kwa ajili ya watanzania walionipa dhamana na walioniweka hapa.