Barnaba Aongelea Uteuzi wa Jokate.
Msanii wa muziki wa bongo fleva kipaji bora kutoka THT , Barnaba classic amefunguka na kumpongeza sana mwanadada Jokate Mwegelo kwa kuteuliwa kuwa mkuu wa wilaya ya kisarawe na kusema kuwa hiyo ni moja ya hatua kubwa ambavyo nchi yetu inapiga kwa kutambua michango wa watu katika tasnia.
Akiongea na simple katika kipindi cha break, Barnaba anasema kuwa amefurahia uteuzihuo lakini anawaona wale ambao wanamsema na kumponda na hata kuchukia utezi wa jokate ni wapumbav na wamekuwa wakipoteza muda wao kufanya kitu kama hicho.
Nampongeza sana Jokate kwa uteuzi, na kwa wale ambao wamekuwa wakimsema vibaa naona ni wapumbavu tu, wapumbavu tena sana kwa sababu kama mtu una kazi zako za kufanya huweiz kukaa na kumsengenya mtu, nasema ni wapumbavu mara mbili.
Mwanadada Jokate anatarajiwa kuripoti na kuapishwa na mkuu wake wa mkoa katika kituo chake cha kazi.