Barnaba Atangaza Ujio Wa Albamu Yake Mpya

Mwanamuziki wa muziki wa Bongo fleva Barnaba Elias maarufu kama Barnaba Classic ameweka wazi kuwa anategemea kutoka na albamu yake mpya hivi karibuni.

Barnaba anayefanya vizuri na ngoma yake ya ‘Chausiku’ aliyomshirikisha Vanessa Mdee amesema kuwa Albamu Yake inatarajia kutoka hivi karibuni aliyoipa jina la ‘Gold’.

download latest music    

Albamu ya muimbaji huyo ambayo inakwenda kwa jina la Gold itakuwa na nyimbo zipatazo 18. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ndipo ameeleza kukamilika kwa albamu hiyo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Barnaba amesema:

Narudia tena kusema hii ni Gold na mgodi umebeba dhaabu ambazo zimepikwa muda mrefu sana, sitaki kusema mengi I can’t wait kwa kweli“.

Hapo mwanzoni  albamu hiyo ilipangwa kutoka February 2018 lakini ikahairishwa hadi July 2018 kutokana na kile Barnaba alichoeleza kuwa wadhamini wake wakuu watatu walipendelea hivyo.

Wasanii waliotajwa kuwepo katika albamu hiyo ni pamoja na Juliana Kanyomozi na Jose Chameleon kutoka Uganda. Kutoka Bongo kuna Vanessa Mdee, G Nako, Ben Pol, Aslay, Barakah The Prince, Linex na Joh Makini.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.