BASATA Kuwashughulikia Diamond na Rayvanny Baada Ya Kupiga ‘Mwanza’

Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) linefungukia kitendo cha Wasanii wa Bongo fleva Diamond Platnumz na Rayvanny kuperfom wimbo wao wa Mwanza ambao umefungiwa.

Mwezi uliopita Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) walitangaza kuufungia rasmi wimbo wa ‘Mwanza’ kwa madai kuwa wasanii hao wamekiuka maadili ya Kitanzania kwa maudhui ya wimbo huo.

download latest music    

Diamond aliimba wimbo huo alioshirikishwa na Rayvanny jana Desemba 15, 2018 katika tamasha la Wasafi lililofanyika jijini Mwanza jana, huku maelfu ya mashabiki wakimshangilia na kumfuatisha alivyokuwa akiimba. Mkali huyo wa Bongo Fleva aliimba wimbo huo  akiwa pamoja na Rayvanny.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Katibu mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza alifungukia ishu hiyo na kusema:

Nimepigiwa simu kuhusu hii kitu. Niko Arusha kikazi nimeshawasiliana na mwenyekiti wa bodi (ya Basata).

Basata itakuja na majibu muafaka kwani hapa (Diamond) kaonyesha kiwango cha juu cha dharau kwa baraza, bodi, wizara (Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo) na Serikali kwa ujumla”.

 

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.