BASATA Wafungukia Tuhuma Za Kumlipisha Diamond Kibali Cha Kwenda Kwenye Birthday Ya Tiffah

Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) limekanusha taarifa za kumlipisha staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz kibali cha kwenda South Africa kwa ajili ya birthday ya mtoto wake Tiffah.

Wiki iliyopita BASATA ilitangaza utaratibu mpya kuwa wasanii wote wanatakiwa kuripoti ofisi  za BASATA kabla ya kusafiri kwenda nchi za nje kwa ajili ya kulipia vibali.

download latest music    

BASATA wamekanusha Tetesi zinazoenea Kwenye mitandao ya kijamii na kudai hawajamlipisha Diamond kibali cha kwenda South Africa kwani kibali hicho sio cha Safari binafsi.

Tunapenda kuutarifu umma kuwa taarifa inayosambaa kwamba Msanii Diamond anatakiwa kuchukua kibali BASATA kwenda kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa mwanaye si ya kweli.

Vibali vya wasanii kwenda nje havihusiani na safari binafsi. Tunazidi kuwakumbusha wasanii kufuata taratibu zote wanapoenda kufanya maonesho nje ya nchi“.

Diamond ametangaza kufanya bonge la party nchini South Africa kwa ajili ya kusheherekea miaka mitatu ya kuzaliwa ya mwanae Tiffah.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.