BASATA Wakanusha Taarifa Za Kuwafungulia Diamond na Rayvanny

Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) limekanusha taarifa za kuwafungulia wasanii Diamond Platnumz na Rayvanny wanaotumikia adhabu ya kutojihusisha na muziki kwa muda usiojulikana baada ya kufanya makosa mbalimbali ndani ya kipindi cha miezi miwili.

Taarifa hiyo imekuja baada ya msanii Diamond kutangaza kwenye mkutano wa waandishi wa habari jana kuwa wameruhusiwa kufanya tamasha la muziki, Wasafi Festival’  nchini Kenya.

download latest music    

Siku chache zilizopita wasanii hao kupitia mtandao wa Instagram Walionekana wakifanya mkutano na waandishi wa habari nchini Kenya kutangaza maonyesho yao yanayoendelea, lakini alifajiri taarifa ya Basata ilisema kuwa hawajatoa ruhusa kwa wasanii hao.

Baada ya kauli hiyo kutoka kwa wasanii hao kutoka WCB, BASATA walitoa tamko lao na kusema:

Ikumbukwe kuwa Desemba 18 tuliwafungia kutojihusisha na sanaa kwa kipindi kisichojulikana kwa kuimba kwa makusudi wimbo Mwanza tulioufungia kwa sababu za kimaadili,

“Baraza linasisitiza kuwa halijawafungulia wasanii hao, pia linawaonya kuacha kutoa taarifa za uongo kabla halijawachukulia hatua kali zaidi,” imeeleza barua hiyo.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.