Batuli Afungukia Ukimya Wake Bongo Movie

Msanii wa filamu za kibongo, Yobnesh Yusuf maarufu kwa Jina la usanii kama Batuli amefunguka na kuweka wazi sababu za kukaa kimya kwa muda mrefu.

Batulia amefunguka na kudai kuwa kukaa kwake kimya na kutosikika mara kwa mara hasa Kwenye skendo za mitandao ya kijamii kutawapa hamu mashabiki zake za kuona filamu zake na kumtunzia heshima.

download latest music    

Kwenye mahojiano yake na gazeti la  Ijumaa Wikienda, Batuli alisema alikaa kimya kwa muda mrefu kwa sababu kuna vitu alikuwa anaviweka sawa kisha arudi tena kwenye ulingo wa filamu na anashukuru Mungu amevikamilisha.

Kutoonekana mara kwa mara kumeniletea heshima hata kwa mashabiki wangu. Kuonekana kila wakati inasababisha watu wanakuchoka, ni bora ukae kimya, ukiwa na kitu ndiyo unaibuka tena na ndivyo wanavyofanya hata wenzetu wa nje”.

Wasanii wengi wa Bongo movie wamekuwa wako takes kwa kutawala vichwa vya habari kwa skendo zao kuliko kazi zao.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.