Batuli: Nitairudishia Heshima Bongo Movie

Muigizaji wa Bongo movie Yobnesh Yusuf maarufu kama Batuli amefungka na kusema ana mipango ya kuirudisha tasnia hii ya Bongo movie kwenye chati.

Kiuweli kabisa Bongo movie imepoa sana kwani ni tofauti na miaka mitano nyuma ambapo kila mtu alikuwa anatazama filamu za Bongo movie lakini hivi sasa hakuna kitu.

download latest music    

Lakini Batuli amekiri kuwa pamoja na Tasnia ya Bongo movie kupoteza muelekea yupo tayari Kupiga na kufanya na kupona kwa ajili ya kuifufua na kuhakikisha anaitudisha pale ilipokuwepo kwenye chati.

Batuli amefunguka hayo Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers ambapo amekiri Bongo movie imepoteza mwelekeo kutokana na kazi mbovu walizokuwa wanazitoq ambazo hazikuwa na viwango sahihi na baada ya kufanya uchunguzi wamejipanga kuwaletea Watanzania kazi bora kabisa.

Filamu au tamthiliya ni biashara kama zilivyo nyingine na biashara yoyote lazima uangalie soko linataka nini kwa sababu wakati tulionao sasa ni tofauti na ule wa zamani, mashabiki wanataka kazi bora na siyo uchafu kwenye runinga zao hivyo nitarudisha heshima ya Bongo Muvi kutokana na kazi ninazokuja nazo”.

Kumekuwa na jitihada nyingi za wasanii mbali mbali wa Bongo movie kuongea kuhusiana na mipango ya kuhakikisha Bongo movie inarudi pale ilipokuwepo na mashabiki pia ni muhimu kutoa sapoti kwa kazi nzuri.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.