Beka Fleva: Mbosso Hajanitetemesha, Aslay Nayeye Acha Tushindane

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayefanya vizuri na ngoma yake ya Kiben10 amefunguka na kusema hajatetemeshwa na ujio mpya wa msanii Mbosso kutoka WCB lakini pia Aslay atashindana naye tu.

Beka fleva, Aslay, Mbosso na Bella waliunda kundi la Yamoto band waliojipatia umaarufu miaka ya nyuma lakini baada ya kuwa pamoja kwa miaka kadhaa kundi hilo liliishia kuvunjika na kila mmoja alishika njia yake na kuanza solo careers.

download latest music    

Wasanii wote wamekuwa wakifanya vizuri na kukubalika na kila mmoja wao amekuwa akidai hakuna uhasama kati yao na kila mmoja anamtakia heri mwenzake na mafanikio.

Lakini pia Beka fleva ameongelea tetesi za yeye kukasirikia mafanikio ya Mbosso kusainiwa WCB na hivyo kusababisha kutohudhuria halfa yake ambapo amedai alichelewa kupata taarifa za shughuli hiyo hali iliyopelekea kushindwa kufika.

Beka fleva amefunguka kuwa alivyoona Utambulishi wa Mbosso kwenye bonge la hoteli la Hyatt Regency na baadae kijamii uwanjani Mwembeyanga hakutetemeshwa hata kidogo ndio kwanza alifurahi kuona mafanikio ya mwenzake lakini pia amesema anafurahia ushindani wake na Aslay kwani unaleta mziki mzuri.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.