Belle 9- Dogo Janja Ndio Anatakiwa Kuchapwa

Msanii wa muziki wa Bongo fleva Belle 9 ameibuka na kudai kama kuchapwa anatakiwa kuchapwa Dogo Janja sio yeye.

Wiki iliyopita Dogo janja Kwenye Interview yake alisema Belle 9 anahitaji kuchapwa viboko 70 baada ya kusema Hamuelewi na hata nyimbo zake anzoimba huwa hazielewi.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Enews ya EATV, Belle 9 amemjibu Dogo na kusema inabidi achapwe yeye kwani nyimbo yake mpya ya ‘Banana’ ni ngoma ya kihuni na hajaielewa:

Nilivyosema msanii ambaye simuelewi ni Madee sikuwa na maana mbaya na samahani kama wamekasirika lakini niliongea kwa uzuri maana ni msanii ambaye huwa namuangalia.

Kusema ukweli nilivyosikia anasema nichapwe viboko nilicheka sana na huenda tunatofautiana kufikiria na labda kwa mazingira aliyokulia yeye anaona kuchapwa viboko kunaweza kumbadilisha mtu ila sio pointi sana maana mambo yamebadilika.

Halafu kama ni viboko anatakiwa achapwe yeye kwa nyimbo anazoimba zenye  utata kwani nyimbo iliyopita alivaa kama mwanamke na nyimbo yake mpya ya Banana anaimba sijui your my Banana na wote tunajua Banana ina maana gani”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.