Ben Breaker Asema Hawezi Kutoka Kimapenzi na Wema Sepetu
Mwanamitindo na mcheza dance maarufu Ben Breaker amefunguka na kusema kuwa kamwe katika maisha yake hajawahikuwaza kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Wema Sepetu kutokana na sababu kuwa akifanya hivyo itakuwa ni kama amemsaliti rafiki yake.
Akijibu swali alilokuwa ameulizwa kuhusu ukaribu wake na wema sepetu , ben amesema kuwa ni kwa sababu ya uhusiano wa kimapezni kati ya Idris na Wema ndio uliomfanya yeye kuwa na mahusiano ya karibu na Wema.
Ben Breaker ansema kuwa pamoja na kwamba yuko karibu na wema lakini hawezi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanadada huyo kwa sababu alishjawahi kuwa na mahusiano na rafiki yake mkubwa idris sultani hivyo akifanya hivyo ni sawa na kwamba amemsaliti rafiki yake na amekuwa akimheshimu sana.