Ben Pol aeleza sababu mahusiano yake huwa hayadumu

Image: Ben Pol na mwanae, Mali

Msanii mkali wa Bongo Ben Pol ni mmoja wa wanaume ambao mashabiki hutamani. Yeye ni mwanaume ambaye anajitambua ila kulingana na yeye mahusiano yake huwa hayadumu.

Ben Pol alifunguka kwa mara ya kwanza kudai kuwa mahusiano yake ambayo yalidumu sana ni pale ambapo alikaa na mwanamke kwa miezi 9 lakini wakaachana.

download latest music    

Kulingana na yeye warembo wengi huja na matarajio ambayo yeye hawezi fikia. Ben Pol ameiambia Choice FM.

“Miezi tisa ndio longest relationship kwa sababu unajua yaani nimekutana na watu wa aina tofauti, watu ambao wanaokuwa na expectation kubwa zaidi kuhusu mtu flani, kwa hiyo akiingia kwenye maisha yako anakuwa ana vitu tayari ali-picture kwamba Ben Pol tutakuwa tunakula bata every weekend, tunakula bata milioni, tunaenda huku na kule. Kwa hiyo mtu anaingia kwenye maisha yako anakuta si mtu wa hivyo ni staa ndio lakini we don’t go to club mara kwa mara, we don’t do this, we don’t do that, kwa hiyo mtu anakuwa disappointed anatoka kwenye mahusiano ndio hicho nime-experience zaidi kwenye mahusiano yangu yaliyopita,”

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua