Ben Pol aweka picha akiwa nusu uchi, mashabiki nao wamponda

Ben Pol hataki mchezo na iwapo haujaziona picha zake mpya basi hautaelewa ninacho sema. Kwa Mara ya kwanza msanii huyu wa nyimbo za RnB ameachia picha zake akiwa uchi lakini anaonekana kama ameketi huku akificha sehemu zake za nyeti.

Picha hizi aliziweka kwenye mtandao wake wa Instagram na mashabiki wake ambao hakuwa wanatarajia jambo kama hili walimshambulia kwa meneno ya kumtusi na wengine wakimueleza kuwa amepoteza muelekeo wake ikiwa hii ndio ndio njia ameamua kuichukua.

download latest music    

Yeye ndiye msanii wa kwanza wa kiume Bongo kuachia picha kama hizi. Hapo mbeleni wengi walikuwa wamemzoea kuweka picha kama amejivalia nguo zake za designer lakini kwa sasa inaonekana kuwa ameamua kufanya mambo mapya.

Mtindo huu sana sana hutumiwa na wanawake lakini Ben Pol ameamua kuonesha kuwa pia wanaume Wanaweza pia. Iwapo haujaiona picha hiyo basi itazame hapa.

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua