Ben Pol aweka wazi kwa nini hataki kuongelelea maisha yake ya kibinafsi kwa sasa

Muimbaji wa bongo, Ben Pol amefunguka kudai kuwa kwa sasa hataki watu wamuulize kuhusu maisha yake ya kibinafsi wala mahusiano yake, Ebitoke na mtoto.

Hii ni kwa sababu ya kazi anayoifanya kwa sasa. Akizungumza kwenye mahojiano, Ben Pol alisema;

download latest music    

“Kwa series ya kazi zangu zinazokuja ningependa sana vitu binafsi nisiviongelee zaidi au hadi pale nitakapokuwa tayari kuzungumzia Ben Pol anafanya nini sasa hivi nianze kuzungumzia,”

Akaendelea kwa kusema;

“kwa hiyo sipo comfortable sana kusema vitu binafsi mahusiano, sijui mtoto nataka kupunguza kuvizungumzia hivyo vitu kwa sasa hivi kusema kweli,”

 

About this writer:

Pauline Syombua

Content Developer IG: Kermbua