Ben Pol- Tetesi Za Darassa Kutumia Madawa Ya Kulevya Sio Za Kweli

Mwanamuziki wa Bongo fleva Darassa alibamba sana siku za nyuma na kibao chake cha ‘Muziki’ ambacho kilikuwa ni kikali balaa lakini siku za hivi karibuni sifa hiyo njema aliyokuwa nayo imekumbwa na wingu baya.

Tetesi za Darassa kujiingiza Kwenye matumizi ya madawa ya kulevya zilisambaa kama moto wa kifuu baada ya picha yake tata kusambaa Kwenye mitandao ya kijamii na kuzua sintofahamu.

download latest music    

Ben Pol ni moja kati ya watu wa karibu wa Darassa na hata amefanya naye kolabo mbili ambazo ni Muziki na sikati Tamaa.

Kwenye Interview ambayo Ben Pol amefanya na Clouds Tv, amesema hamsini taarifa hizo kwani anawasiliana naye karibia kila siku.

Kusema kweli siamini, sina element yoyote inayonifanya niamini chochote kuhusiana na hizo tetesi kwa sababu ili mtu uweze kusema kitu lazima uwe na element ambazo umeziona lakini mimi hamna element.

Mimi tunaongea masaa mawili, saa zima kwenye simu, video call sometime kwa hiyo sioni kuna element ya hicho kitu”.

Wasanii wengi walikuwa wanafanya vizuri tumeona jinsi wanavyoteketea kisa matumizi ya madawa ya kulevya ambayo kwa kiasi kikubwa yameathiri maisha yao mfano mzuri ni Q Chillah,Ray C na Chid Benz na wengineo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.