Bifu La Gabo Na Duma Bado Linafukuta

ingawa wenyewe wanasema kuwa hawana ugomvi lakini kumekuwa na kurushiana kwa maneno baina ya wasanii wa Bongo movie kati ya Duma na Gabo Zigamba, bifu ili lilianza pale ambapo Duma alianza kwa kumponda sana Gabo na kumwambia kuwa hajui kuvaa, hata hivyo Duma amekuwa akikerwa na tabia ya Gabo kukaa kimya kwa muda mrefu bila kufanya filamu ili kikudhi kiu ya mashabiki zake.

Duma amekuwa akisema kuwa hana ugomvi wowote na Gabo ila tu anajaribu kumuweka sawa msanii mwenzie kwa sababu ni moja ya wasanii wa Bongo movie mwenye mashabiki wengi wanaopenda kazi zake, lakini ili aendelea kuwaweka msahabiki zake na kuwaongeza ni lazima  ajitaidi kutoa filamu mpya ili kuwafanya mashabiki waaendelee kumsapoti.

download latest music    

Hivi karibuni Duma alifunguka na kusema tena kuwa msanii Gabo amekwa akibweteka tu katika kufanya kazi, hayo yamekuja baada ya msanii Duma kufanya uzinduzi wa filamu yake ya ‘bei kali’, ambapo Duma alimualika Gabo katika uzinduzi huo lakini Gabo hakutokea.Akiongea na waandishi wa habari Duma nasema kuwa kilichomsikitisha ni kwanini Duma aliamua kutokutokea katika uzinduzi huo ilhali alipewa mwaliko.Kwa mujibu wa Duma, anasema kuwa katika sehemu kama hizo ndipo wasanii wanapopata nafasi ya kukutana na mashabiki wake na kujifunza mambo mengi anayohusiana na filamu kwa sababu kuna kuwa na mkusanyika wa watu wengi hivyo kuna mengi ya kujifunza.

alipopata nafasi ya kuongea na kuelezea kwanini gabo hakuonkana katika uzinduzi huo, msanii duma alisema “yeye kutokuwepo anakosa vitu vingi sana,gabo anashuka kimasoko,mimi na yeye hatuna mugogoro wowote ila tu tunaelezana ukweli wa mambo ilitueze kutoa tasnia hapa ilipo na  kuipeleka sehemu nyinginw.mimi simkosei heshima kwa sababu sijamkosea kitu chochote kwa sababu sijawai kumtukana tusi hata moja,Gabo ana mashabiki wengi  sana yeye anabweteka  tu, no man, fanya kazi” ameongea Duma

Inawezekana ikawa ni njia ambayo Duma anaitumia kukuza tasnia ya filamu lakini, nadhani njia inayokuwa bora zaidi ni wawili hao kukaa pamoja na kumaliza tofauti zao ili kuunda mbinu itakayokuwa bora ya kukuza tasnia hiyo kwa pamoja.

 

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.