“Bila Wewe Sijiwezi Rashid Wangu” Shamsa Ford Afunguka Baada ya Kutangaza ni Mjamzito

Muigizaji wa Bongo movie Shamsa Ford amezidi kushika kasi katika mitandao ya kijamii baada ya kutangaza rasmi kuwa yeye na mume wake Rashid ‘Chiddi Mapenzi’ wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

Shamsa amekuwa muwazi kuwa anampenda sana mume wake pamoja na changamoto wanazopitia ambapo ni juzi tu Shamsa alisema rasmi kuwa hata kama mume wake akichepuka na kutembea na wanawake wengine hawezi kumuacha.

download latest music    

Miezi michache iliyopita Chiddi Mapenzi alikumbwa na skendo mitandaoni baada ya kudaiwa kutoka kimapenzi na moja ya wasichana maarufu instagram ambaye anaitwa Irene lakini Shamsa alisema pamoja na kuchepuka hawezi kumuacha.

Shamsa ametumia ukurasa wake wa Instagram kutangaza kuwa anatarajia kupata mtoto wake wa kwanza na mumewe Chiddi baada ya kumuita baba kijacho ambapo aliandika ujumbe huu:

I wish ningekuwa na neno la ziada la kukwambia zaidi ya nakupenda…… Bila  wewe sijiwezi Rashidi wangu….. Mwenyezi Mungu mume wangu halali baba K wangu”.

Wiki chache zilizopita Shamsa aliweka wazi kuwa alibeba mimba ya kwanza ya Chiddi lakini kwa bahati mbaya ikatoka kutokana na kupata stress za hapa na pale.

Huyu atakuwa mtoto wa pili kwa Shamsa ambaye tayari ana mtoto mwingine anayeitwa Terry aliyezaa na mumewe wa zamani lakini atakuwa mtoto wa kwanza kwa Chiddi na Shamsa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.