Bill Nas Akana Bifu na Dogo Janja Baada Ya Kumwagiana Povu Zito

Msanii wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya kuchana William Lymo maarufu kama Bill Nas amefunguka na kuweka wazi kuwa yeye na msanii mwenzake Dogo Janja hawana bifu lolote.

Tetesi za Bill Nas na Dogo Janja kusemekana kuwa na bifu zilianza mara baada ya wawili hao kurushiana maneno ya kejeli Kwenye mitandao ya kijamii ambapo Dogo Janja alimtania Bill Nas kwa kuachwa na mwanamke wake kwa sababu ya mdomo  na Bill Nas alimchana kuwa ameolewa na Uwoya ili acheze na mtoto wake.

download latest music    

Global Publishers lilimtafuta Billnass ili azungumzie ishu hiyo ambapo alisema hana bifu na Dogo Janja bali maneno hayo yalikuwa ni utani tu.

Sina bifu na Dogo Janja, hayo maneno tuliyokuwa tunaandikiana yalikuwa ni utani tu, sisi tumeshazoea kutaniana kwa hiyo nawaomba mashabiki zangu wasichukulie kwamba tuna tofauti”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.