Bill Nas Athibitisha Kuwa Yupo ‘Single’ Kwa Sasa

Msanii wa muziki wa Bongo fleva anayefanya vyema kabisa na hit single yake ya ‘Labda’ William Lymo maarufu kama Billnas ameweka wazi kuwa kwa sasa hana mpenzi yaani ni Single Boy.

Bill Nas amefunguka na kudai hivi sasa yupo single hana mwanamke Lakini pia kinacho mtatiza ni kwamba bado hajajua ni mwanamke gani ambaye anatakiwa kuwa naye Kwenye Mahusiano.

download latest music    

Kwenye mahojiano aliyofanya na Star Showbiz, Bill Nas amesema kwamba hahitaji kukurupuka, anachotamani ni kupata mtu sahihi ili aweze hata kufunga naye ndoa na si kuwa kwenye uhusiano ambao unaanza leo na kumalizika kesho.

Watu wanaweza wasiamini lakini ukweli ni kwamba kwa sasa sina uhusiano wa aina yoyote ile. Kinachonikwamisha kuingia ni kwamba sioni bado mwanamke sahihi wa mimi kuwa naye.

Ninasubiri pengine Mungu anionyeshe, huyo nitakayempata ndiye atakuwa mke wangu na sihitaji uhusiano wa kuanza leo na kuvunjika kesho”.

Bill Nas alishawahi kuwa Kwenye Mahusiano na msanii mwenzake Faustina Charles maarufu kama Nandy lakini wawili hao waliachana siku za nyuma kidogo.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.