Bill Nas Hawezi Kumfikia Ngwea- TID

Mkongwe wa Muziki wa Bongo fleva khalid Mohamed na maarufu kama TID ameibuka na kuweka wazi kuwa marehemu Ngwea alikuwa msanii mkali hata Bill Nas hawezi kumfikia.

Ikiwa ni siku chache tangu Ngwea atimize miaka kadhaa tangu Kifo chake TID ambaye alikuwa rafiki yake mkubwa ameweka wazi kuwa pengo lake halitaweza kuzibwa na msanii yoyote.

download latest music    

Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha habari TID amesisitiza hata Bill Nas hajaweza kumfikia Ngwea kwa kipaji alichokuwa nacho enzi za uhai wake:

Hakuna msanii anayeweza kumfikia Ngwea that man was special Ngwea alikuwa blessed alafu umfananishe na nani? Bill Nas anaweza kuwa a half of it lakini hawezi kuwa kama Ngwea, Ngwea can rap Ngwea can sing Ngwea can give you melody halafu unataka kumfanisha na mtu? Hakuna wa kufanana naye”.

TID na Billnas walishawahi kuwa Kwenye bifu zito miaka ya nyuma lakini bifu hilo lilimalizika baada ya kutoa pamoja wimbo unaoitwa ‘Ligi Nzito’.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.