Bill Nas- Nandy ni Dada Yangu na Ninamuheshimu Sana

Msanii wa Bongo fleva aliyefanya vizuri na ngoma zake kama chafu pozi amefunguka na kusema Nandy ni dada yake na anamuheshimi sana.

Bill Nas na Nandy walishangaza watu wengi wiki chche zilizopita baadae ya kuitana dada na kaka huku Ikiwa wazi kabisa kuwa wawili hao walisha wahi kuwa Kwenye Mahusiano siku za nyuma.

download latest music    

Bill Nas ameiambia Enews ya EATV kuwa uamuzi wake wa kumuita Nandy dada unatokana na ukweli kuwa mapenzi yao yalipiita siku nyingi sana kwani baada ya kuachana na Nandy alikuwa Kwenye uhusiano na wasichana wengine wawili hivyo kwake sio Ex tena bali ni dada:

Kwa kweli kibusara Nandy ni dada yangu inaweza pia kiumri akawa dada yangu ingawa sina uhakika lakini ni dada kiheshima kwa sababu sijawahi kumvunjia heshima kwa namna yoyote ile ndio maana nikamuita dada lakini sio kindugu”.

Bill Nas na Nandy walizua gumzo mwezi uliopita baada ya video yao ya ngono kuvuja Kwenye mitandao ya kijamii.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.