Bill Nas: Sio Lazima Kila Mtu Ajue Mahusiano Yangu

Mwanamuziki wa Bongo fleva anayetamba kwa hivi sasa na ngoma yake ya ‘Tagi bovu’ amefunguka na kusema yeye sio msururu sana lakini anaona kuna baadhi ya vitu ambavyo anaona hamna umuhimu kuvianika na kila mtu ajue.

Bill Nas ametengeneza sana headlines kwenye mitandao ya kijamii wiki mbili tatu tangu atoke ngoma yake lakini kama kawaida kilichokuwa kinamfanya aongelewe sana ni mahusiano yake ya kimapenzi.

download latest music    

Kuna tetesi zilizosambaa toka mwaka jana na kudai kuwa Bill Nas ana Mahusiano ya kimapenzi na msanii mwenzake kutoka THT Nandy habari ambazo siku zote wawili hao wamezikataa na kusema wao ni marafiki.

Kwenye Interview aliyofanya na Dizzim Online, Bill Nas amekataa taarifa zilizodai kuwa yeye ni msiri sana hasa linapokuja suala la mahusiano yake na mpenzi wake ambapo Bill Nas amekiri hapendelei kuanika Mahusiano Yake hadharani:

Kusema ukweli mimi sio kwamba ni msiri sana ila hivi ndivyo nilivyo sio lazima kila kitu kila mtu ajue ama wafahamu kuna vitu watu wanapaswa kama binadamu waheshimu privacy yako na kuna vitu unatakiwa ubaki navyo mwenyewe au watu wako wa karibu”.

Bill Nas amekiri kuwa ana mpenzi wake lakini hayupo tayari kumuweka wazi kwa sasa na hizi skendo za yeye kutoka na wasanii wenzake zinakuwa kama zinamuharibia mapenzi yake.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.