Billnas Afunguka Kuhusu Ndoa Yake na Jinsi Ali Kiba Alivyohusika

Mwanamuziki wa Bongo fleva Bill Nas amefunguka na kuweka wazi kwa nini alitangaza ndoa yake mapema mwaka huu.

Bill Nas aliungana na wasanii wengi ambao wametangaza wanatarajia kuuaga ukapera hivi karibuni na kufunga ndoa.

download latest music    

Kwenye Interview yake na Wasafi Tv, Bill Nass amesema kuwa anaamua kuoa kutokana anapenda familia, pia wasanii wanatakiwa kuwa kama watu wengine kwani kufanya hivyo haimaanishi msanii atashuka kimuziki.

Niliposti kuhusu kuoa na pia kuhusu nani nitamuoa nitaamua mimi sio mtu mwingine. Mtu kama Alikiba anaweza kuoa na game yake bado ipo strong kuna kila haja, na pia inatambulisha kwamba ndoa ni jambo muhimu lakini pia sisi ni wasanii na ni watu kama wengine”.

Lakini pia Bill Nas ameweka wazi kuwa siku aliyohudhuria Harusi ya msanii mwenzake Ali Kiba alizidi kupata morali ya kuoa baada ya kuona jinsi mtoto wake alivyokuwa na furaha:

Mtoto wake alikuwa happy sana kwenye ile harusi kwa hiyo ile ilini-impress zaidi”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.