Billnas Afungukia Mahusiano Yake na Ali Kiba

Mwanamuziki wa Bongo fleva Billnas amefunguka na kuweka wazi kabisa uhusiano wake na staa wa Bongo fleva Ali Kiba.

Billnas amerudi Kwenye headlines huku safari hii Ikiwa ni uhusiano wake wa kikazi na Ali Kiba. Siku chache zilizopita kuna taarifa za sintofahamu zilisambaa kumuhusu Billnas na Ali Kiba.

download latest music    

Kwenye mahojiano na Kipindi cha Kikaangoni cha East Africa Tv, Billnas amefunguka kuhusu tetesi zilizodai kuna ngoma kati yake na Alikiba inakuja.

Nina Mahusiano mazuri na Ali Kiba na huwa ananishauri mambo mengi katika kazi zangu na hata muda mwingine huwa tunataniana naamini anakubali kazi zangu maana huwa nikiachia ngoma ananiambia mdogo wangu hapo freshi au kazia buti sehemu fulani.

Sitaki kuliweka sana hilo mbele ila watu wajue tunayo mahusiano mazuri kama nilivyo na mahusiano mazuri na wasanii wengine“.

Billnas anayefanya Muziki wake katika miondoko ya kurap anafanya vizuri hivi sasa na ngoma yake ya ‘Tagi Ubavu”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.