Billnas- Nipo Tayari Kufanya Kazi BASATA Ili Kuikoa Sanaa

Staa wa Bongo fleva na Hitmaker wa wimbo wa ‘Labda’ Billnas amefunguka na kuweka wazi kuwa Yupo Tayari kufanya kazi BASATA (Baraza la Sanaa Tanzania).

Billnas ambaye mbali na kuwa ni msanii mzuri lakini pia ni msomi kwani alihitimu elimu yake ya Chuo Kikuu mwaka jana.

download latest music    

Billnas amefunguka na kuweka wazi kuwa a naomba Kupitia elimu yake ya chuo kikuu apatiwe kazi BASATA ili aweze kutatua migogoro inayoendelea kati ya wasanii na BASATA.

Kwenye mahojiano na kipindi cha Refresh cha Wasafi Tv, Billnas amesisitiza kuwa wasanii wanahitaji mtu wa kuwawakilisha ili mawazo yao yafike katika uongozi:

Mimi natamani sana kufanya kazi pale BASATA ili niweze kushirikiana nao kutengeneza miundo mbinu sahihi ya kuweza kuwasaidia wasanii kuliko makatazo, masharti magumu, kuigandamiza sanaa nahisi wakinipa nafasi na vyeti vyangu kuna kitu tunaweza tukatengeneza”.

Lakini pia Billnas alisisitiza kuwa hataki hiyo kazi kwa ajili ya kupata mshahara mkubwa bali anajitoa ili kusaidia BASATA kufanya maamuzi yatakayo wafaidisha wasanii na kazi zao:

Sitaki hiyo nafasi kwa ajili ya kunufaika ila natafuta njia ili wasanii wote tuweze kunufaika na pia maprodyuza, waandishi, madancer na hata waigizaji kwa sababu sanaa sio kitu cha mchezo”.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.