Billnass Atoa Sababu ya Kumpenda Sana Mama Yake.
Msanii wa bongo fleva Bilnass amefunguka na kutoa sababu ya kuwa siku zote amekuwa akimtaja sana mama yake kuliko baba yake na kwamba hata katika moja ya wimbo wake alionekana kumpondea baba yake.
Billnas anasema kuwa amekuwa akifanya hivyo ili kuwapa moyo na motisha wamama wote na kujiona kuwa wao ni bora zaidi ili kufanya kazi vizuri kwa bidii.
Namsifia sana mama yangu ili kuwapa motisha wanawake wengine na kuendelea kupambana zaidi, sio kwamba baba yangu sio bora zaidi hapana lakini baba yangu ni mtu mzuri na amekuwa akinisaidia sana na ni mtu mzuri na anaendelea kunisaidia tu na yupo kwa ajili yangu kila siku na huwa siona kama kuna haja ya kumtaja baba kwa sababu inajulikana kuwa baba ni kichwa cha familia.