Brown Mauzo Yupo Tayari Kuwa Spea Tairi Kwa Wema Sepetu

Msanii maarufu kutoka Mombasa Kenya Brown Mauzo amefunguka na kudai ana mapenzi mazito kwa Muigizaji wa Bongo movie Supastaa Wema Sepetu.

Kwenye mahojiano yake na kipindi cha Enews cha East Africa Tv, Brown amesema kuwa amekuwa akivutiwa sana na Wema Sepetu na yupo tayari muda wowote kumuoa mrembo huyo hata kama ikibidi awe spea tairi.

download latest music    

Mimi namzimia sana Wema Sepetu kwa bahati mbaya sijawahi kuonana naye namzimiaga sana, kila mtu anasema ukweli kutoka moyoni kila shetani na mbuyu wake. Licha ya kwamba alikuwa na nani sijui na nani ila mimi nipo tayari kumuoa, na popote atakapokuwa namwambia mimi nampenda na nataka kumuoa.. hata kama akiwa na mtu mwingine mimi nipo tayari hata niwe spea tairi”.

Brown amemwagia Wema Misifa kibao huku akidai ni mwanamke ambaye amekaa na ameona anafaa kuwa mke wake wa ndoa.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.