Bushoke Amkingia Kifua Q-Chillah
Msanii wa muziki wa kitambo kidogo, bushoke amefunguka na kumtetea rafiki yake ambae pia ni msanii mwenzake q-chillah na kusema kuwa sio kweli kuwa alishawahi kuja kulala kwake kwa sababu ya kuishiwa au kuwa na maisha magumu kama watu wamekuwa wakizusha kwa sababu kwa jinsi anavyomju rafiki yake huyo ana uwezo wa kulala sehemu yoyote kwa kuamua.
Akiongea na eNews, bushoke anakanusha taarifa za kuwa Q-chillah alipoachana na mwanamke wake aliamua kwenda kukaa kwake kama kujiifadhi kutokana na kuwa hakuna na sehemu maalum ya kukaa kwa kipindi icho ivyo aliamua kumpa hifadhi .
Q-chief hajawahi kuja kukaa kwangu na ikitokea anakaa kwangu basi ujue kaja kupiga stori tu na sio kwamba ana shida ya kulala.kuna watu wa kawaida ambao hawawezi kukosa sehmu ya kulaa, q-chillah hawezi kukosa sehemu ya kulala,ni maamuzi tu ya leo akalale wapi na anaweza hata akaenda kulala anapopataka maana anaweza kwenda kulala hata Nairobi.