Calisah Atangaza Kumiliki Kampuni ya Kuwapa Mimba Wanawake.
Mwanamitindo calisah amefunguka na kutangaz kuwa kwa sasa ana kampuni mbili kubwa ambazo ni ya kukuza vipaji vya wanamitindo wachanga lakini pia kampuni kubwa nyingine aliyokuwa nayo ni ya kuwapa wanawake mimba ambao wamekosa mimba kwa wanaume wengine.
Mwanamitindo huyo anasema kuwa mpaka sasa ameshafanikiwa kuwapa mimba wanawake kama 25 swala analofanya ni kumtafuta na kusainia nao mkataba na kulipana baada ya hapo mnaingia ndani na kukamilisha kazi yenu.
Mwanamitindo huyo alishawahi kufunguka na kusema kuwa wanawake weng wamekuwa wakimtumia meseji na kumtaka kimapenzi huku wengine wakitamani sana kuzaa nae kutokana na muonekano wake na ndio maana ameamua kuanzisha kampuni hiyo.