Casto Adai Yuko Tayari Kuitwa Mjinga Kwa Penzi La Tunda

Mtangazaji wa Clouds Tv, Casto Dickson amefunguka mazito ya moyoni juu ya mpenzi wake Tunda na kudai yuko tayari kuitwa mjinga kwa ajili ya penzi la binti huyo.

Hii ni mara ya kwanza Casto Kuvunja  ukimya tangu mtoto wake Patrick aliyezaa na Muna kufariki wiki chache zilizopita.

download latest music    

Casto amefunguka hayo siku mbili zilizopita ambapo ilikuwa ni birthday ya mpenzi wake Tunda na kuweka wazi mapenzi yake makubwa aliyonayo kwake.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Casto aliandika maneno haya:

Acha Dunia inione mi KOLO/MJINGA Ila ur my Wife to be Happy Birthday my T.. God Bless u”.

Ujumbe huo wa Casto umepokelewa kwa hisia tofauti na mashabiki zake ambao wengi wao wamemvaa kwa kumuongelea Tunda lakini hajatoa Kauli yoyote kwa utata unaoendelea juu ya mwanaye Patrick.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.