Casto Athibitisha , Tunda Amepokelewa Kwao.
Mtangazaji wa Clouds tv, Casto Dickson amesema kuwa kwa upande wa wazazi wake hakuna mwenye shida na maamuzi yake ya kuwa na mahusiano na mwanadada tunda kama watu wanavyokuwa wakiwatukana katika mitandao ya kijamii.
Akiongea na mwandishi mmoja wa habari casto anasema kuwa “uzuri mimi baba yangu huwa anaheshimu kile nilichoamua, ukijumlisha na kile nilichoamua na ushauri anaoutoa yeye kila kitu kipo sawa tu,my father hana wasiwasi na nilichokiamua na my mom alishafariki muda mrefu lakini naamini huko alipo anaona kuwa nilichokiamua ni sahihi.
Casto na tunda wapo katika mahusiano kwa muda mrefu sasa na kumekuwa na maneno mengi ya kuwashambulia kutokana na kuamua kwao kuwa katika mahusiano huku wengi wakijaribu kuangalia maisha ya nyuma ya mwanadada Tunda.