Cathy Ajivunia Uamuzi Wa Kutokutoa Mimba na Kuwa na Mtoto Mkubwa Sasa

Muigizaji mkongwe kwenye tasnia ya Bongo movie Sabrina Rupia maarufu kama Cathy amewashangaza watu wengi Baada ya kumuonyesha Mtoto Wake wa kwanza.

Cathy alizua taharuki Baada ya kuweka wazi Siri yake kuwa ni mama wa Mtoto mkubwa tu wa kiume ambaye anaitwa Issa mwenye umri wa miaka kumi na Sita kwa sasa.

download latest music    

Kijana huyo aliibua mshtuko hivi karibuni baada ya mama yake  huyo kuanika picha wakiwa pamoja na watu kujiuliza Cathy alimzaa akiwa na umri gani.

Kwenye mahojiano aliyofanya na Global Publishers, Cathy ameweka wazi kuwa alimzaa mtoto wake huyo akiwa na miaka 16 hivyo hivi karibuni ndiyo yalikuwa mahafali yake ya kuhitimu digrii ya kwanza ndani ya Chuo Kikuu cha Sokoine, Morogoro.

Huyu ni mtoto wangu wa kwanza, nilimpata nikiwa na miaka 16, namshukuru Mungu sikumdhuru kama mabinti wengi wanavyofanya wakipata mimba za utotoni, sasa nafurahia yaani ndiye huyu tumekua wote, nampenda sana, ni mwanangu, ni kaka yangu, ni mshauri wangu, kifupi ndiyo kila kitu kwangu“.

Ni kawaida kwa mastaa kuficha watoto wao na kudanganya kuwa hawana watoto kwa kuhofia umri wao halisi kujulikana mfano ni mastaa Kama Johari Chagula na Lulu Diva ambao wameshawahi kupata  skendo za kuficha Watoto.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.