Chid Benz Akamatwa Tena Kwa Madawa ya Kulevya

Msanii mkongwe wa kizazi kipya Chid Benz, amekamatwa tena  kwa mara nyingine  mkoani Dodoma akiwa na mke wake kwa tuhuma za kukutwa na madawa ya kulevya aina ya Heroine.

Sio mara ya Kwanza kwa msani Chid Benz kukamatwa na madawa ya kulevya lakini pia msanii huyo kwa zaidi ya miaka mitatu sasa amekuwa akipelekwa katika vituo mbalimbali kwa ajili ya kutibu watu waliathirika na madawa ya kulevya.

download latest music    

Mkuu wa kituo cha polisi mkoani Dodoma amethibitishwa kukamatwa kwa msanii huyo  tangu tarehe 30 Desemba mwaka 2017, lakini mpaka sasa wapo mahabusu.

Chid Benz ambae amekuwa akisaidia na watu mbalimbali katika tasnia ya muziki ili aweze kuinuka na kurudi tena kwenye muziki ili aweze kujikwamua katika tatizo hilo lakini jitihada hizo zimeonekana kukwama kabisa.

About this writer:

Expedicto Lilian

#Godseeker, I am what i ought to be and always i will be, but am not what i used to be.