Chid Benz Akamatwa Tena na Madawa Ya Kulevya

Mkongwe wa Muziki wa Bongo fleva Rashidi Makwito maarufu kwa Jina la usanii kama Chid Benz amejikuta Tena mikononi mwa vyombo vya sheria baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya.

Chid Benz ambaye amekuwa akikataa kutumia madawa ya kulevya na kudai ameacha tangu atoke sober house amekamatwa tena madawa kama ilivyokuwa mwaka jana.

download latest music    

Chid Benz amekamtwa na Jeshi la Polisi jijini Dodoma kwa tuhuma za kukutwa na mzigo wa bangi kiasi cha gramu tano.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto amesema hayo leo Jumatatu, Juni 18, 2018 wakati akizungumza na wanahabari jijini humo baada ya kumtia mbaroni msanii huyo.

Hii ni mara ya pili kwa Chidi kukamatwa na madawa ya kulevya huku akidai kuwa alishaacha kutumia madawa hayo na anaendelea na matibabu Sober House.

Hii ni sehemu ya taarifa ya polisi kuhusu kukamatwa kwa watuhumiwa mbaliombali akiwemo Chidi.

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.