Chid Benz Bado Hajajutia Kutumia Madawa Ya Kulevya

Msanii mkongwe wa Bongo fleva anayefanya miondoko ya hip hop, Chid Benz amesema pamoja na kwamba alijiingiza katika matumizi ya madawa ya kulevya lakini hajawahi kujuta.

Chid Benz ambaye amekuwa akitumia madawa ya Kulevya kwa miaka kadhaa sasa amefunguka na kudai kuwa hajawahi kujutia kitu chochote Kwenye maisha yake.

download latest music    

Chid Benz amefunguka hayo Kwenye mahojiano na Wasafi Tv ambapo ameweka wazi kuwa hajawahi kujutia kutumia madawa kwa sababu mashabiki wake wamekuwa nae bega kwa bega Kwenye kila jambo.

No! no!, tusiongelee mambo ya madawa maisha ndio yapo hivyo, hamna kitu ninachojutia. Siwezi kujutia nilikolabo na wasanii, siwezi kujutia yaliyonikuta, siwezi kujutia mabadiliko yangu, siwezi kujutia chochote kilichonipata.

Zaidi naona nikijutia mashabiki wangu wataona Chidi vipi why wewe hujutie wakati sisi tunaendelea kukupenda hadi leo. Ukitangaza show TMK unajaza, Morogoro, Singida unajaza, unajutia nini”.

Chid Benz ameshapelekwa rehab mara kadhaa ili aweze kuachana na matumizi ya madawa hayo lakini imekuwa ngumu kwani amesharudi Kwenye matumizi hayo mara zote.

 

About this writer:

Diana

I am a hard working young woman Aspiring writer with dreams larger than life itself, always living by the principle that live today like there is no tomorrow.